Dizasta Vina – A muscular Feminist

Dizasta Vina A muscular Feminist

Dizasta Vina – A muscular Feminist Lyrics

Artist: Dizasta Vina
Song: A muscular Feminist

Dear boys dear… men
Ni sisi wasichana kina dada, mabinti na mama zenu
Tunaongea kutoka upande wa chini, upande mbali upande kutoka usawa wenu
Upande nilipo msichana kuna hitilafu

‘So’ sikio lako thabiti ni ushindi kwangu
Ninayotaka kusema hapa sio siri katu
Ili ujue nina vingi vya ku-offer kabla ya mwili wangu
Kwa miaka mingi nimeishi gizani

Gizani kwenye baridi na miba mingi nyikani
Eneo uliotaka niishi ni eneo kandamizi
Na bahati mbaya we’ ndo’ mchoraji wa hii ramani
Ramani inamwonyesha binti kama chombo cha mapenzi

Msindikizaji mtoto tegemezi
Ramani isiyojua vituo
Isiyojua tunaweza kuwa marafiki bila kuvuana nguo
Dear boys, dear men

Mngeelewa mngeiweka fikra sahihi
Kama sanaa jinsi inavyozalisha fasihi
Mi’ ni mlezi ukinivika mi’ umeivika jamii
U-gentlemen sio kulipa mgahawani

Umeshapitwa na wakati
Hainisaidii kunifungulia mlango nikifika kwenye gari
Nifungulie fikra nitafakari
Dear boys, dear men

Tumekuwa tegemezi maana mmeficha mbegu
Nani wa kuipigana vita yetu
Umbali kati yetu utakuwa mkubwa milele
Maana si ni wahanga wa mifumo mliyoiunda wenyewe

Nikijaribu kusoma nabaki bure
Maana unajali mwili wangu, ndo’ maana sitaki shule
Kila nikienda popote wanaomba ngono
Labda niwe changudoa to the fullest

At least I’ll get paid
Hata sisi tuna life too
And the world doesn’t revolve around you
Nipo tofauti sikupenda, na tena

Unaponichezea fahamu kuwa ninazeeka mapema
Shujaa unakumbukwa mzazi sikumbukwi
Na kwanini kuwa msafi sio haja kwako
Au kutembea kifua wazi ni kujiamini

Nikitembea mimi ni nusu uchi
I wish ungejua pride yako nayo sumu
I wish ungejua kuwa uanaume sio nguvu
I wish ungejua kuwa binadamu hajakamilika

Mwanaume aliyekamilika anatimiza majukumu
I wish ungejua kuwa na mimba sio haya
I wish ungejua mwanamke kuwa kichwa si vibaya
I wish ungejua kuwa upendo nao una nguvu kwahiyo mwanamke akitongoza mwanaume si malaya

I wish ungejua kuonyesha fear sometimes, it’s okay
It’s okay kulia sometimes
I wish ungejua uongozi hauoni jinsia si
Tatizo mwanamke kuongoza njia sometimes

Mifumo mliyoianzisha ina maisha
Na chenye maisha kin#z#kwa
Kwahiyo ipo siku mwanamke atasimama
Na vita tunayopigana tutashinda

Inasikitisha hamkui kihisia, japo mnakua kiakili
Natamani … natamani mngejua kuwa inauma sana kuwa namba mbili kwenye kila nyanja
Ego ni power ila iogope
Maana ni upanga unaokata pande zote

Ngoma nzuri ngoma nzuri haitavuma milele
Ukitumia ubabe vibaya utakuvunja mwenyewe
Hadithi ya mwanamke alimshawishi Adam kula tunda
Iliandikwa na wewe

Sijui Delilah alichukua nguvu za mumewe akaziuza
Iliandikwa na wewe
Upande wangu wa hadithi haujasikilizwa
Pengine hautasikilizwa hasirani

Maana ulianzisha shule akasoma mwanaume
Mwanamke nikabaki nyumbani
Dear boys, dear men
Hamtakaa kwenye kilele

Maana kilele ni kuwa mama
Mi’ ni kichwa sio wewe ungekuwa kichwa
Mtaani kusingekuwa na single mothers
Lini mtaacha kutuita mademu

Au labda mwite demu mama’ako
Ukiona hauwezi naomba niheshimu kwa maana heshima inaanza kwako
Na haja ya maelewano iko hapo
I mean… ipi salama ya kichwa cha familia bila

Mkono wa kuosha macho?
Najua tupo tofauti
Na tofauti yetu itabaki, itabakia hivyo milele
Ila naomba usinichukie nielewe

Dear boys, dear men
Ni sisi wasichana, kina dada, mabinti na mama zenu
Tunawasilisha kutoka upande wa chini upande wa pili
Upande mbali kutoka usawa wenu

Dear girls, dear Women
Ni sisi kina kaka, kina baba, wanaume machizi wenu
Tunaongea kutoka upande wa juu, upande wa mbali
Upande uliowekwa na asili yetu

Upande wenye mafungu yenye ulanguzi
Upande wenye uthubutu na maamuzi
Upande wenye machozi jasho na damu
Uongozi upako ufahamu, upande usio na uhuru na uchaguzi

Upande uliofanya wanaume tutengwe na tunu
Tutengwe na tunu
Upande ambao pengine kuishi wewe ni ngumu
Upande ambao asali yake ni kilele cha sumu

Upande ambao haushabikii tija ya upendo au furaha au amani
Kama hauangalii pima utagundua upande niliosimama mimi ni ngao ya jamii nzima
Uanaume sio ushindi ni jukumu
Uanaume sio rizki ni hukumu

Ungejua kwanini wanaume wana msongo wa mawazo pengine ungefurahia udogo wako
Dear women , dear girls
Mmekuwa chombo cha ngono
Maana mmetufanya chombo cha fedha

Kama nguo hazitabadili mishono
Hatuwezi kuwa marafiki bila ngono nawaeleza
Mnapoona padogo pana taswira ndefu
Kiasi haujui si ndio tuliopigana vita yenu

Hata mkiamka mmekuwa wanaume leo
Mtagundua kuwa jinsia sio cheo
Wapendwa tukishindana mtashindwa
Hata mkishinda ushindi wenu hautalindwa

Kama ambavyo kila mmoja anatumia choo chake
Kila mmoja a-play role yake na awe bingwa
Dear women
Ndoa sio mafanikio

Kuna wengi wanakonda maana ndoa zao sio
Ndoa ni mwiba usijivune
Ukiipata niamini unaweza kukamilika bila mume
Dada baki shule bila elimu utateseka

Ukitegemea urembo ipo siku utazeeka
Kama ukiweka mwili wako hisani
Ukizeeka tutajali ulichonacho kichwani
‘Skiza’ hata wanaume tuna doubts too

And this world doesn’t revolve around you
Tuna stress zinatufunga na tena
Kazi zetu ni ngumu ndo’ maana tunakufa mapema
Kama unahisi upo huru umepotoka

Hauwezi kuwa huru wakati umelipiwa posa
Dear women
It’s okay kuwa namba mbili
Majukumu sio mashindano acha kukalili

It’s okay kumlea mwanaume asiye na kazi
Ukaendelea kumuheshimu bila kumshusha hadhi
Mbona sisi tunalea wanawake masikini wamekata ringi na bado mtaani hatutatangazi
Mwanaume ana jukumu la kujenga msingi?

No, msingi unajengwa na elimu
Kwa mfano nani anayekubali kucheza uchi kwenye videos? Jiheshimu nikuheshimu
Urembo pia ni power, ila ni power na iogope
Maana ni upanga unaokata pande zote

Ngoma ya uzuri haitovuma milele
Ukiutumia urembo vibaya utakuvunja mwenyewe
I wish ungejua unachowaza ni muhimu
Ukifanyia kazi na kuwa wa kwanza si’ majibu

I wish ungejua kwamba asili imenipa umwamba
Nikulee, kukulea wewe ni msaada si’ wajibu
I wish ungejua tuko tofauti hata utunge dini
Hauwi mwamba kwa kumweka mwanaume chini

I wish ungejua kuwa kichwa ni hukumu
Maana hakuna kinachotisha kama jukumu
Wangapi tumelelewa na hao single mothers
Maskini and we turned out just fine

Maybe idea ya kuacha kujali mtoto sababu
Baba mjinga ingeachwa far behind
Tunasubiria uhalisi ubadilike
Labda uhalisia haubadiliki huu

Labda ni wakati wa kukubali ili yaishe kwamba
Mtoto ni wa mama na baba ni rafiki tu
Lini mtaacha kutuita madanga ma-sponsors? Ndio, niheshimu nikuheshimu nitaacha wewe
Ukiona imetosha, au sio?

Najua tuko tofauti
Na tofauti itabaki hivyo milele
Usinichukie nielewe
Dear girls, dear women

Ni sisi kina kaka kina baba, wanaume machizi wenu
Tunawasilisha kutoka upande wa juu, upande mbali uliowekwa na asili yetu
Find more lyrics at https://dcslyrics.com

You can purchase their music thru
DCSLyrics.com Amazon Music    DCSLyrics.com Apple Music
Disclosure: As an Amazon Associate and an Apple Partner, we earn from qualifying purchases

A muscular Feminist Lyrics – English Translation

Dear dear boys … men
We girls are sisters, daughters and your mothers
We speak from the bottom, on the far side from your balance
I am a young side for errors

‘So’ ear me steady is victorious
I want him to say this is not a secret never
To know I have many ku-offer before my body
For many years I have lived in darkness

Darkness in winter and many th#rn# wilderness
The area is an area repressive want to live
And unfortunately we ‘membrane’ painter of this map
Map shows daughter as an instrument of love

Escort dependent child
Map which knows no stations
Which knows no we can be friends without clothes kuvuana
Dear boys, dear men

You should realize you had thought it appropriate
How art produces a far as literature
Mi ‘is the guardian you clothed me mi’ has clothes the community
U-gentlemen do not pay restaurant

Umeshapitwa and time
Hainisaidii kunifungulia I arrived at the car door
Help me thinking I think
Dear boys, dear men

We have been dependent for ye hide seeds
Who’s our war kuipigana
Distance between us will be the largest ever
For systems not victims you’re working on themselves

If I tried to read Nabaki free
For consideration for my body, membrane ‘I do not want school
Whenever I go anywhere they ask for sex
Maybe I should changudoa to the fullest

At least I’ll get paid
But we have a life too
And the world does not revolve around you
I’m different I like, and again

Unaponichezea know that I grow old sooner
Hero is remembered parent I remembered
And why do not need you to be clean
Or walk bare chest is confident

I’m walking around half naked
I wish you knew your pride have formed
I wish you would know that manhood is not strong
I wish you would know that the human is incomplete

The man who commissioned it fulfills obligations
I wish you would know that this is not pregnant
I wish you would know that the woman’s head is not wrong
I wish you would know that you love them so powerful a man not a woman who made passes prostitute

I wish you knew showing fear Sometimes, it’s okay
It’s okay to cry Sometimes
I wish you would know the leadership does not see gender not
Problem Sometimes a woman leading the way

An initiating systems has life
And illuminating life buried
So there is a day a woman will stand
And we will win the battle we fought against

Sadly not grow emotionally, even though you grew up mentally
I wish … I wish you would know that it hurts to have two numbers on all fronts
Ego is power but Fear
For sword cutting truths are round

Good dance the best dance ever shall sound
Using the wrong authoritarianism will break yourself
The story of the woman seduced Adam to eat fruit
It was written by you

I do not know Delilah took the power of her husband sell
It was written by you
My side of the story is ujasikilizwa
Perhaps it is sinister utasikilizwa

For a school founded recited man
Woman I stayed home
Dear boys, dear men
Hamtakaa on top

For the summit is to be a mother
Mi ‘is not a title you would head
Mtaani there would be single mothers
When will you stop calling us Mademu

Or maybe call girlfriend mama’ako
If you feel you can not respect me because I ask you to respect begins
And the need for compromise is that
I mean … what the head of the family safe without

Hand washing eyes?
I know we’re different
And our differences remain, will remain so forever
Except that I do not understand nichukie

Dear boys, dear men
It is us girls, sisters, daughters and your mothers
We communicate from the bottom on the other side
Turn away from your balance

Dear girls, dear Women
Are we deep brothers, fathers, men of your Machizi
We speak from the top side, the far side
Side set by our nature

The side portions with trafficking
Side with assertive and decisive
Side with blood sweat and tears
Leading anointing aware, side without freedom and choice

Toward that made men tutengwe and values
Tutengwe and values
You probably live side who are hard
Whose side it is the culmination of honey poisoning

Side who ushabikii productivity love or joy or peace
If the measure does not look the part, I realized I was standing the whole community shield
Virility is not winning role
Virility is not a judgment rizki

If you know why men have depression would probably enjoy your littleness
Dear women, dear girls
You have become a tool for sex
For you have made a financial tool

If the clothes do not change stitches
We can not be friends without sex nawaeleza
When you see a little wider long images
The amount does not know is that we fought you

Even when you wake up you have to be men today
You’ll notice that gender is not a title
Hello we contend will fail
Even if you win you win it You’ll be protected

As everyone is using his toilet
Each a-play his role and be a champion
Dear women
Marriage is not successful

There are many lean mean their marriage is not
Marriage is not to be arrogant thorn
Exposure should I believe can be completed without husband
Dada left school without education will suffer

Based on the old beauty exists day
If you put your body a favor
Ukizeeka will not care what you have scalp
‘Attn’ even men have doubts too

And this world does not revolve around you
We stress again zinatufunga
Our task is tough membrane ‘meaning we die early
If you feel you’re free to come out

You can not
Find more lyrics at https://dcslyrics.com

Dizasta Vina Lyrics – A muscular Feminist

Please support our site by sharing it.
And please follow our site to get the latest lyrics for all your favourite songs.

Please support the artist and us by purchasing your favourite music thru our Amazon Music and Apple Music links 🙂

You can purchase their music thru
DCSLyrics.com Amazon Music    DCSLyrics.com Apple Music
Disclosure: As an Amazon Associate and an Apple Partner, we earn from qualifying purchases

From the album:
The Verteller [Explicit]
Release Year: 2021